Machapisho

INJILI YA YESU JIONI

NAO WANIABUDU BURE!

Nawasalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu kristo, Na karibu tujifunze maarifa ya mbinguni. Siku tunazoishi ni siku za mwisho, Bwana alisema atakuja kama Mwivi! Sio kwamba anakusudia kuja namna hiyo ili kutukomoa kwamba tusiende mbinguni; bali ni kwa sababu watu wapo gizani, wamelala usingizi wa kiroho, hao ndio atawajilia kama mwivi. watakuwa hawajui majira ya kujiliwa kwao. watakuwa wametingwa na shughuli na masumbusu ya mali. watalewa na mali, watalewa na mvinyo, watakuwa walafi wa mambo ya dunia. 4 Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi. 1 Wathesalonike 5:4 Walio katika nuru wataitambua siku hiyo. Mwivi huja wakati mwenye nyumba amelala, na kama angekesha asingeibiwa. Ndio maana sisi wenyewe tukeshao; hapa haimaanishi mikesha, bali Kutokusinzia kiroho. Usilale kiroho usiku na mchana. Na Siku inayozungumziwa hapo ni siku ya Unyakuo wa kanisa . Lakini watu wengu kutokana na mafundisho ya wanadamu; hawajui jambo hili na wengine wamesikia na kuamini ku...

UMEMKATAA MUNGU KAMA WAISRAELI PASIPO KUJUA!

Neema ya kristo na iwe nanyi; karibu tujifunze hekima ya Mungu itupayo uzima wa milele. Israeli baada ya kufika kaanani wakitokea misri, walikuwa chini ya waamuzi. Hawakuwa na mfalme bali Mungu ndiye alikuwa mfalme wao akiwatumia waamuzi. Lakini BWANA akijua utafika wakati waisraeli watataka mfalme kama jinsi yalivyo mataifa yasiyomcha Mungu yanavyofanya. Hivyo alimpa Musa maagizo kuwa watakapotaka mfalme waruhusiwe kumweka mfalme ambaye Bwana atamchagua (kumb 7:14-15). Ilifika wakati mmoja, Samweli kama mwamuzi wa wakati ule aliona amezeeka na hivyo akawateua wanawe wawaamue Israeli badala yake. Wanawe hawakwenda katika njia ya haki hata kuwafanya Wazee wa israeli wamwendee Samweli ili kumsihi awafanyie mfalme kama ilivyo kawaida ya mataifa mengine. (1samweli 8:4-5) , jambo lile halikumpendeza Samweli. Lakini aliende kumsihi Mungu juu ya ombi lao na Mungu vile vile alighadhabishwa na shauri lile kutoka kwa wale wazee. Akasema; 1samweli 8 7Bwana akamwambia samweli, isikilize sau...

NA TUMFANYE MTU KWA MFANO WETU!.

Hujambo? karibu tujifunze maarifa ya mbinguni. Kanisa limepita katika nyakati mbalimbali, tumeanza na nyakati za EFESO yaani wakati wa injili ya mitume, huko kote hutaona wanataja Mungu kuwa ni utatu wala ana nafisi tatu mpaka baada ya madhehebu kuanza. Pale ambako kughoshi injili kulipoanza na nafsi tatu zikaanza. Biblia inasema baadhi ya maandiko yalifungwa yasijulikane katika ufahamu wa mwanadamu hadi wakati wa mwisho ambao ni nyakati za LAODIKIA. Nyakati hizi zilianza miaka ya 1900 na zitakoma baada ya unyakuo tu. Kwa hiyo siri hizi zinakuwa zinafunuliwa nyakati hizi, madhehebu hayakubaliani na ufunuo huo maana yametoka rohoni na kuingia mwilini na kukalili mapokeo. Madhehebu yanafuata zaidi theolojia inasema nini na sio Mungu anasema nini! Kama tungefuata Mungu anasema nini hakuma mtu angejiita M-KATOLIKI, M-TAG, M-FPCT, M-EAGT, M-ANGLICAN N.K. Sawa na 1kor 1:12-13, 1kor 3:4. Mgawanyiko huu umetufanya kulikaribisha giza kwa sehemu maana tunaamini tu theolojia yetu inasemaje na ...

JE! NAWEZA KUWA SAFI NAMI NINA MIZANI YA UDHALIMU!!

Jina la Yesu litukuzwe, Mungu wetu ni Mungu mmoja na jina lake ni Yesu. JINA LAKE LITUKUZWE!!! Karibu tule na kunywa pamoja. Kwa wapendwa wote katika Kristo na wasio katika kristo, nawasalimu! Siku hizi ni siku za mwisho, Na ni wakati wa kujitakasa sana na uovu wa dunia hii maana kweli imepotoshwa na watu wakachagua kuuamini uongo na kukataa kweli, Hiyo namaanisha wakristo kuwa vuguvugu, jambo ambalo ni baya kuliko mtu asiyeamini. Mika 6:11 JE! NAWEZA KUWA SAFI NAMI NINA MIZANI YA UDHALIMU, na mfuko wa mawe ya kupimia ya udanganyifu? Kuna mambo mengi yalikuwa yanaendelea katika Yuda wakati nabii Mika anahubili habari hizi, Yuda ilikuwa imeacha njia ya Bwana na kulinajisi taifa. Wakati huo pia alikuwapo nabii isaya, na mika alihubili na kutabili Yuda kwenda utumwani, Babeli (mika 4:10). Yuda ilionywa kwa mda mrefu kwa kurudi nyuma kwa matendo yasiyo haki, ni kweli walikuwa kanisa la Mungu teule ambao Mungu aliwachagua kwanza kama mzaliwa wa kwanza, wakati huo kanisa lilipoa, wakaan...

UWE NA UTUNGU, UTAABIKE ILI UZAE!

Jina la Bwana litukuzwe, Salaam wapendwa! Karibuni katika chakula cha kiroho. Umewahi kufikilia maumivu gani mwanamke hupata wakati wa utungu? Amewekewa sharti apate utungu ili azae tangu alipoasi Edeni kama moja ya laana Bwana aliyoitoa. Sasa katika unabii mwanamke huwakilisha Kanisa. Tazama kwa makini katika kanisa; Utagundua kuwa jinsi mwanamke alivyo katika jamii ndivyo kanisa lilivyo. Angalia hilo utaliona katika nyakati zote zilizopita na uje uangalie Mwanamke wa sasa na kanisa la Sasa lilivyo. Jinsi mwanamke alivyojiharibu ndivyo kanisa lilivyo (ukahaba, uzinzi, uasherati, mavazi(matendo) machafu n.k), kanisa pia lina tabia za namna hiyo. Nataka tutazame amri ya utungu kwa mwanamke na kuzaa kwa taabu, Amri hii ni kwa kanisa pia. Tazama kanisa la kale yaani israel; jinsi Mungu alivyolitoa katika hatia ya misri ya kuabudu sanamu(uasherati). Akaliposa na kuwa mke kwa Bwana. Licha ya kwamba Bwana alikuwa nao kuwaongoza njia kufika kanaani lakini aliwapitisha katika maumivu chungu...

MADHARA YA KUTOKUWA NA KIU YA KUMJUA KRISTO

Nakusalimu katika jina la Yesu, mwokozi na Mungu wetu.Karibu tujifunze na ili tuzidi kukua katika kimo cha ujuzi na maarifa. Unafahamu unavyoshikwa na kiu ya maji jinsi utakavyohangaika kuyapata, waswahili hadi wakasema maji ni uhai wakimaanisha umuhimu wake katika mwili ambapo husema 70% ya mwili ni maji. Mtu anaweza kwenda hadi wiki tatu bila chakula lakini ni siku tatu tu anweza kukaa bila maji. Kila mtu alishawahi kushikwa na kiu, kuna ile kiu inakushika halafu unakuwa mbali na maji kwa wakati huo; huwa inanyima raha kabisa. Ulishawahi kunywa soda kama mbadala wa maji?? kimsingi soda ni kimiminika kama maji isipokuwa ina kemikali yenye radha fulani ya utamu tofauti na ilivyo katika maji , ila cha ajabu soda huwa haindoi kiu, bali hutuliza dakika kadhaa kiu inarudi palepale, sijui kwa nini maana soda ni maji. Hebu tuulete mfano wa kiu hiyo kiroho, mwili unahitaji maji kuzima kiu lakini mtu anao mwili na Roho. Kila roho imeumbiwa kiu ya ibada ama kuabudu, ndio maaana utakuta hata...

WANA JUHUDI YA KUMTAFTA MUNGU LAKINI SI KATIKA MAARIFA!

Nawasalimu katika jina la mwokozi wetu. Karibu tujifunze maarifa ya mbinguni ambayo wengi huangamia kwa kuyakosa. Mimi ni mwanafunzi wa Yesu, nami nakushudia katika habari hizi za ufalme wa mbinguni kuwa ni njema na hupaswi kuzikosa. Maana uangamivu wa dunia upo karibu. Siku hizi za mwisho kuna mambo mengi yalitabiliwa kutukia, mojawapo ni kuwa watu wa kujipenda wenyewe, Upendo kupoa(upendo wa kumpenda Mungu) Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, 2 Timotheo 3:2 Haya yote yanatukia kila kukicha na ni dhahiri mbele za macho yetu, hatuhitaji kusimuliwa. Baada ya kuingia injili ya manabii wa uongo, hayo mambo yaliyotajwa yakapata nafasi kanisani/hekaluni. Kuna jambo hapa nataka ulipate/ulielewe, kwamba Hekalu la Mungu linapaswa kuwa takatifu na Hekalu ni kuanzia mwili wako. 16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa nda...

MCHUNGAJI HARUHUSIWI KUGOMBEA UONGOZI WA KISIASA SERIKALINI

Nakusalimu rafiki na ndugu yangu katika kristo Yesu. Bwana asifiwe! Tufurahi katika Bwana tukijua majina Yetu yameandikwa katika kitabu cha mbinguni; sio vinginevyo! Tusifurahi kwa sababu sisi tunasifiwa makanisani kuwa watoaji wazuri ama waimbaji wazuri ama walimu wazuri ama wenye upako. Yote hayo hata anayekwenda motoni huyapata tena na zaidi. Lipo jambo katika siku hizi za mwisho kwamba mtu kuwa mhudumu yaani kuwa na huduma inamfanya kujiona wa kipekee. Tena Mungu pale anapomtumia kwa viwango katika karama aliyowekewa hutaka kana kwamba Dunia yote imtambue na ajulikane pote; Sio Mungu ajulikane bali yeye ajulikane! Kuna machaguo mawili tu tuliyopewa yaani Mungu ama shetani. Badala ya Baraka ni laana. Sasa, KUNA IMANI KUU MBILI DUNIANI; yaani kumwabudu Mungu wa kweli na nyingine ni kinyume cha hiyo. Kumwabudu Mungu asiye wa kweli inajumuisha WAPAGANI NA VUGUVUGU. Yesu ndiye Mungu hivyo anayeabudu nje ya Yesu huyo ni mpagani pia. Maana roho ya mwanadamu imeumbiwa ibada ndani, ...

NIMEWAPELEKEA TAUNI KAMA YA MISRI (CORONA) LAKINI HAMKUNIRUDIA MIMI

Picha
Nakusalimu katika Jina la Yesu kristo. Tumshukuru Bwana maana fadhili zake ni za milele. Mungu wetu ni mmoja na Jina lake ni YESU(YEHOVA MWOKOZI). Kuna mitazamo mingi kuhusu ugonjwa wa CORONA, wengine wakisema ni uzushi, wengine wakisema ni njama za Kutafta New (one) world govt kwamba chanjo yake itaambatana na kuwekewa microchip (TRACKING DEVICE). Na wengine ni watumishi wa Mungu (mitume na manabii wa hiari) wakasema wamewekwa kwa ajili ya saa kama hii na Wakatabili ugonjwa huo hautafika Tanzania; lakini ajabu ukafika na watu wakaendelea KUWAINUA na Kuwasifu (Luka 6:26) Hiyo ni baadhi ya mitazamo, lakini kwangu mimi CORONA ni tauni kutoka kwa Bwana(hasira ya Bwana) juu ya maovu yetu. Nakumbuka katika ndoto 30/5/2020, niliota ugonjwa ugonjwa ule umenipata na hali yangu ilikuwa ya kawaida na wala sikuwa na hofu yoyote; wakati huo alikuwepo kondakta wa daladala mmoja tumekaa naye tukimsubili konda mwenzake ambaye alikuwa ametoka na ndio nilikuwa namdai chenji yangu iliyonifanya nim...

SIKU ZA MWISHO KUTAKUWEPO NYAKATI ZA HATARI

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu kristo Mwana wa Mungu aliye hai. Neema na Rehema zake ziwe nawe katika nyakati hizi za mwisho. Miaka takribani 2000 iliyopita, Paulo akioneshwa na Roho mtakatifu juu ya siku za mwisho anasema; 1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 2 Timotheo 3:1 Siku za mwisho ni hizi tunazoishi hivi leo. Sifa kubwa ya kanisa la leo (siku hizi za mwisho) ni kuwa VUGUVUGU; yaani si baridi wala moto.. 15 Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. Ufunuo wa Yohana 3:15 16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. Ufunuo wa Yohana 3:16 Kanisa la nyakati hizi ndio ambalo ni vuguvugu, kanisa linaanza kwa mtu mmoja, wanapokuwa wengi huwa na mahali pa kukutania. Kuwa Vuguvugu ni kwenda nusu moto nusu baridi. KANISA LIKISHAMWACHA ROHO MTAKATIFU NDIO HUUNDA DHEHEBU KAMA ILIVYO LEO. Kwa maneno mengine Kuwa moto ...

TOFAUTI KATI YA PETRO NA PAPA

Jina la Bwana litukuzwe. Mpendwa nakusalimu kwa jina la Yesu kristo Bwana wetu. Karibu tuongeze maarifa ili sote tuwe tayari kupokelewa katika Ufalme wa Mbinguni. Wengi huwa hatuelewi kama Madhehebu tuliojifungamanisha nayo tayari tumetengeneza dhambi ya udhehebu. Mara nyingi sana Watu leo hawana haja na Injili ya Toba bali ile nyingine isiyokuwepo katika Maandiko, ila tamaa ya mwanadamu ameileta kwa kufungua mianya; Mwingine kwa ajili ya ukuu Mwingine kwa ajili ya mali Mwingine kwa ajili ya umaarufu n.k. Hayo tuyaache, leo tuongelee hasa Madai ta Dhehebu la Katoliki ambalo hasa hudai ndio kanisa la Mitume. Sitakupa hisyoria nzima ila nitakupa UTOFAUTI KATI YA MTUME PETRO NA PAPA Mara nyingi tumekuwa tukihubili juu ya Mpinga kristo kama ndiye Papa wa katoliki. 3 Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu; 2 Wathesalonike 2:3 4 yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kil...