UDHEHEBU; DHAMBI INAYOPOTEZA WATEULE WENGI.
Shalom Mwana wa Mungu; Karibu katika chakula cha uzima, Neno la Mungu likikaa ndani yako hutaona kiu kamwe! Wapendwa katika Bwana, Tupo mwishoni kabisa katika Majira ya siku za Mwisho. Moja ya siku hizi ambazo tunaruka na kuzurura na Kuyawaza ya dunia Bwana atakuja kama umeme. Ni wakati pekee Bwana atakuja kama Mwizi yaani katika Unyakuo. Alisema tusemapo kuna Amani, Ndipo Uharibifu Uwajiapo 1wathesalonike 5:3 Mwisho wa Dunia Bwana hatakuja kama Mwizi; Hautakuwa wakati wa Amani; Kumbuka Mwisho utakuwa wakati wa Vita, Katika dhiki kuu, siku za giza nene kama ambavyo Nabii Amosi anasema Amosi 5:18-20. 18 Ole wenu! Ninyi mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana? Ni giza, wala si nuru. Amosi 5:18 19 Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu; au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma. Amosi 5:19 20 Je! Siku ya Bwana haitakuwa giza, wala si nuru? Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga. Amosi 5:20 Bila shaka Unaona hapo k...